7. Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’Lakini sijibiwi.Naita kwa sauti kubwa,lakini sipati haki yangu.
8. Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipiteamezitia giza njia zangu.
9. Amenivua fahari yangu;ameiondoa taji yangu kichwani.
10. Amenivunja pande zote, nami nimekwisha;tumaini langu amelingoa kama mti.
11. Ameichochea ghadhabu yake dhidi yangu;ameniona kuwa kama adui yake.
12. Majeshi yake yanijia kwa pamoja;yametengeneza njia ya kuja kwangu,yamepiga kambi kuizunguka nyumba yangu.
13. Mungu amewaweka ndugu zangu mbali nami;rafiki zangu wakuu wamenitoroka kabisa.
14. Jamaa zangu na marafiki hawanisaidii tena.
15. Wageni nyumbani mwangu wamenisahau;watumishi wangu wa kike waniona kuwa mgeni.Mimi nimekuwa kwao mtu wasiyemjua.
16. Namwita mtumishi wangu lakini haitikii,ninalazimika kumsihi sana kwa maneno.
17. Nimekuwa kinyaa kwa mke wangu;chukizo kwa ndugu zangu mwenyewe.
18. Hata watoto wadogo hunidharau,mara ninapojitokeza wao hunizomea.