5. Mnaishusha hadhi yangu mpate kujikuza;mnanilaumu kwa kunyenyekezwa kwangu.
6. Jueni kwamba Mungu amenitendea vibaya,na kuninasa katika wavu wake.
7. Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’Lakini sijibiwi.Naita kwa sauti kubwa,lakini sipati haki yangu.
8. Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipiteamezitia giza njia zangu.
9. Amenivua fahari yangu;ameiondoa taji yangu kichwani.