Yobu 19:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mnaishusha hadhi yangu mpate kujikuza;mnanilaumu kwa kunyenyekezwa kwangu.

6. Jueni kwamba Mungu amenitendea vibaya,na kuninasa katika wavu wake.

7. Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’Lakini sijibiwi.Naita kwa sauti kubwa,lakini sipati haki yangu.

8. Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipiteamezitia giza njia zangu.

9. Amenivua fahari yangu;ameiondoa taji yangu kichwani.

Yobu 19