Yobu 16:9-22 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Amenirarua kwa hasira na kunichukia;amenisagia meno;na adui yangu ananikodolea macho.

10. Watu wananidhihaki na kunicheka;makundi kwa makundi hunizunguka,na kunipiga makofi mashavuni.

11. Mungu amenitia mikononi mwa wajeuri,na kunitupa mikononi mwa waovu.

12. Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja,alinikaba shingo na kunipasua vipandevipande;alinifanya shabaha ya mishale yake,

13. akanipiga mishale kutoka kila upande.Amenipasua figo bila huruma,na nyongo yangu akaimwaga chini.

14. Hunivunja na kunipiga tena na tena;hunishambulia kama askari.

15. “Nimejishonea mavazi ya gunia,fahari yangu nimeibwaga mavumbini.

16. Uso wangu ni mwekundu kwa kulia,kope zangu zimekuwa nyeusi ti;

17. ingawa sijafanya dhuluma kwa mkono wangu,na sala zangu kwa Mungu ni safi.

18. “Ewe dunia, usiifunike damu yangu iliyomwagika;kilio changu kienee kila mahali.

19. Nina hakika ninaye shahidi wangu mbinguni,mwenye kunitetea yuko huko juu.

20. Rafiki zangu wanidharau;nabubujika machozi kumwomba Mungu.

21. Laiti mtu angenitetea mbele ya Mungu,kama ifanyikavyo duniani kati za watu wawili.

22. Naam, miaka yangu ni michache,nami nitakwenda huko ambako sitarudi.

Yobu 16