Yobu 16:16-22 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Uso wangu ni mwekundu kwa kulia,kope zangu zimekuwa nyeusi ti;

17. ingawa sijafanya dhuluma kwa mkono wangu,na sala zangu kwa Mungu ni safi.

18. “Ewe dunia, usiifunike damu yangu iliyomwagika;kilio changu kienee kila mahali.

19. Nina hakika ninaye shahidi wangu mbinguni,mwenye kunitetea yuko huko juu.

20. Rafiki zangu wanidharau;nabubujika machozi kumwomba Mungu.

21. Laiti mtu angenitetea mbele ya Mungu,kama ifanyikavyo duniani kati za watu wawili.

22. Naam, miaka yangu ni michache,nami nitakwenda huko ambako sitarudi.

Yobu 16