19. Mtiririko wa maji hula miamba,mvua kubwa hufanya mmomonyoko wa ardhi.Ndivyo nawe unavyoharibu tumaini la binadamu.
20. Wewe wamwangusha binadamu, naye akatoweka milele;waubadilisha uso wake na kumtupilia mbali.
21. Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari.Wakiporomoshwa, yeye haoni kabisa.
22. Huhisi tu maumivu ya mwili wake,na kuomboleza tu hali yake mbaya.”