Yobu 14:19-22 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Mtiririko wa maji hula miamba,mvua kubwa hufanya mmomonyoko wa ardhi.Ndivyo nawe unavyoharibu tumaini la binadamu.

20. Wewe wamwangusha binadamu, naye akatoweka milele;waubadilisha uso wake na kumtupilia mbali.

21. Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari.Wakiporomoshwa, yeye haoni kabisa.

22. Huhisi tu maumivu ya mwili wake,na kuomboleza tu hali yake mbaya.”

Yobu 14