Yobu 14:18-22 Biblia Habari Njema (BHN)

18. “Lakini milima huangukamajabali hungoka mahali pake.

19. Mtiririko wa maji hula miamba,mvua kubwa hufanya mmomonyoko wa ardhi.Ndivyo nawe unavyoharibu tumaini la binadamu.

20. Wewe wamwangusha binadamu, naye akatoweka milele;waubadilisha uso wake na kumtupilia mbali.

21. Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari.Wakiporomoshwa, yeye haoni kabisa.

22. Huhisi tu maumivu ya mwili wake,na kuomboleza tu hali yake mbaya.”

Yobu 14