Yobu 13:4-8 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Lakini nyinyi mnaupakaa uongo chokaa;nyinyi nyote ni waganga wasiofaa kitu.

5. Laiti mngekaa kimya kabisa,ikafikiriwa kwamba mna hekima!

6. Sikilizeni basi hoja yangu,nisikilizeni ninapojitetea.

7. Je, mnadhani mwamtumikia Mungu kwa kusema uongo?Mnafikiri kusema kwa hila kunamfaa yeye?

8. Je, mnajaribu kumpendelea Mungu?Je, mtamtetea Mungu mahakamani?

Yobu 13