Yobu 12:16-21 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Yeye ana nguvu na hekima;wanaodanganywa na wanaodanganya ni wake.

17. Huwaacha washauri waende zao uchi,huwafanya waamuzi kuwa wapumbavu.

18. Huwavua wafalme vilemba vyao;na kuwafunga viunoni kamba za wafungwa;

19. Huwaacha makuhani waende uchi;na kuwaangusha wenye nguvu.

20. Huwanyanganya washauri kipawa chao cha kuongea,huwapokonya wazee hekima yao.

21. Huwamwagia wakuu aibu,huwaondolea wenye uwezo nguvu zao.

Yobu 12