12. Hekima iko kwa watu wazee,maarifa kwao walioishi muda mrefu.
13. Lakini hekima na uwezo ni vyake Mungu,yeye ana maarifa na ujuzi.
14. Akibomoa, hakuna awezaye kujenga upya;akimfunga mtu, hakuna awezaye kumfungua.
15. Akizuia mvua, twapata ukame;akiifungulia, nchi hupata mafuriko.
16. Yeye ana nguvu na hekima;wanaodanganywa na wanaodanganya ni wake.
17. Huwaacha washauri waende zao uchi,huwafanya waamuzi kuwa wapumbavu.
18. Huwavua wafalme vilemba vyao;na kuwafunga viunoni kamba za wafungwa;
19. Huwaacha makuhani waende uchi;na kuwaangusha wenye nguvu.
20. Huwanyanganya washauri kipawa chao cha kuongea,huwapokonya wazee hekima yao.
21. Huwamwagia wakuu aibu,huwaondolea wenye uwezo nguvu zao.
22. Huvifunua vilindi vya giza,na kuleta mwangani yaliyokuwa gizani.