1. Ndipo Yobu akajibu:
2. “Sawa! Nyinyi ni watu wa hekima.Hekima itakufa wakati ule mtakapokufa.
3. Mimi nami ni mwelewa kama nyinyi.Mimi si mtu duni kuliko nyinyi.Yote mliyosema kila mtu anajua.
4. Nimekuwa kichekesho kwa rafiki zangu:Mimi niliyemwomba Mungu na akanijibu;mimi niliye mwadilifu na bila lawama,nimekuwa kichekesho kwa watu.