9. Kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo.Je, utanirudisha tena mavumbini?
10. Je, si wewe uliyenimimina kama maziwa,na kunigandisha kama jibini?
11. Uliuumba mwili wangu kwa mifupa na mishipa,ukaifunika mifupa yangu kwa nyama na ngozi.
12. Umenijalia uhai na fadhili,uangalifu wako umeisalimisha nafsi yangu.
13. Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni.Lakini najua kuwa hiyo ilikuwa nia yako.
14. Ulikuwa unangojea uone kama nitatenda dhambi,ili ukatae kunisamehe uovu wangu.
15. Kama mimi ni mwovu, ole wangu!Kama mimi ni mwadilifu, siwezi kujisifu;kwani nimejaa fedheha, nikiyatazama mateso yangu.