Yobu 10:7-11 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Wewe wajua kwamba mimi sina hatia,na hakuna wa kuniokoa mikononi mwako.

8. Mikono yako iliniunda na kuniumba,lakini sasa wageuka kuniangamiza.

9. Kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo.Je, utanirudisha tena mavumbini?

10. Je, si wewe uliyenimimina kama maziwa,na kunigandisha kama jibini?

11. Uliuumba mwili wangu kwa mifupa na mishipa,ukaifunika mifupa yangu kwa nyama na ngozi.

Yobu 10