Yeremia 51:17-19 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Kila mtu ni mpumbavu bila maarifa,kila mhunzi anaaibishwa na vinyago vyake;maana sanamu zake ni udanganyifu mtupu,wala hazina pumzi ndani yake.

18. Hazina thamani, ni udanganyifu mtupu;wakati watakapoadhibiwa,nazo zitaangamia.

19. Mungu aliye hazina ya Yakobo si kama hizo,maana yeye ndiye aliyeviumba vitu vyote,na Israeli ni kabila lililo mali yake;Mwenyezi-Mungu wa Majeshi, ndilo jina lake.

Yeremia 51