Yeremia 46:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Lakini mbona nawaona wametishwa?Wamerudi nyuma.Mashujaa wao wamepigwa,wamekimbia mbio,bila hata kugeuka nyuma.Kitisho kila upande.Mwenyezi-Mungu amesema.

6. Walio wepesi kutoroka hawawezi,mashujaa hawawezi kukwepa;huko kaskazini kwenye mto Eufratewamejikwaa na kuanguka.

7. Nani huyo aliye kama mto Nili uliofurikakama mito inayoumuka mawimbi?

8. Misri ni kama mto Nili uliofurikakama mito inayoumuka mawimbiIlisema: “Nitajaa, nitaifunika nchi,nitaiharibu miji na wakazi wake.

9. Songeni mbele, enyi farasi,shambulieni enyi magari ya farasi.Mashujaa wasonge mbele:Watu wa Kushi na Puti washikao ngao,watu wa Ludi, stadi wa kutumia pinde.”

Yeremia 46