23. Niliiangalia nchi, lo! Imekuwa mahame na tupu;nilizitazama mbingu, nazo hazikuwa na mwanga.
24. Niliiangalia milima, lo, ilikuwa inatetemeka,na vilima vyote vilikuwa vinayumbayumba.
25. Nilikodoa macho wala sikuona mtu;hata ndege angani walikuwa wametoweka.
26. Niliona nchi yenye rutuba imekuwa jangwa,na miji yake yote imekuwa magofu matupu,kwa sababu ya hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.
27. Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Nchi nzima itakuwa jangwa tupu;lakini sitaiharibu kabisa.