Yeremia 4:23-27 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Niliiangalia nchi, lo! Imekuwa mahame na tupu;nilizitazama mbingu, nazo hazikuwa na mwanga.

24. Niliiangalia milima, lo, ilikuwa inatetemeka,na vilima vyote vilikuwa vinayumbayumba.

25. Nilikodoa macho wala sikuona mtu;hata ndege angani walikuwa wametoweka.

26. Niliona nchi yenye rutuba imekuwa jangwa,na miji yake yote imekuwa magofu matupu,kwa sababu ya hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.

27. Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Nchi nzima itakuwa jangwa tupu;lakini sitaiharibu kabisa.

Yeremia 4