Yeremia 36:16-19 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Waliposikia maneno hayo yote, walitazamana kwa hofu. Wakamwambia Baruku, “Hatuna budi kumweleza mfalme maneno haya yote.”

17. Kisha wakamwuliza Baruku, “Hebu tuambie, umepataje kuandika maneno yote haya? Je, Yeremia alisema, nawe ukayaandika?”

18. Baruku akawajibu: “Yeye alisema, nami nikawa nayaandika kwa wino katika hati hii.”

19. Kisha wakuu hao wakamwambia Baruku, “Wewe nenda ukajifiche pamoja na Yeremia, na pasiwe na mtu yeyote atakayejua mahali mlipo.”

Yeremia 36