Yeremia 29:5-7 Biblia Habari Njema (BHN)

5. ‘Jengeni nyumba mkae. Limeni mashamba, pandeni mbegu na kula mazao yake.

6. Oeni wake, mpate watoto; waozeni wana wenu na binti zenu nao pia wapate watoto. Ongezekeni na wala msipungue.

7. Shughulikieni ustawi wa mji ambamo nimewahamishia. Niombeni kwa ajili ya mji huo, maana katika ustawi wake nyinyi mtastawi.

Yeremia 29