Yeremia 25:18-20 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Kwanza Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na viongozi wake, ili kuifanya iwe jangwa, ukiwa, kitu cha kuzomewa na kulaaniwa, kama ilivyo mpaka leo. Halafu:

19. Farao, mfalme wa Misri, maofisa na viongozi wake, pamoja na watu wake wote;

20. wageni wote walioishi nchini Misri; wafalme wote wa nchi ya Uzi; wafalme wote wa miji ya Wafilisti, Ashkeloni, Gaza, Ekroni na mabaki ya Ashdodi.

Yeremia 25