Yeremia 2:25-27 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Israeli, usiichakaze miguu yakowala usilikaushe koo lako.Lakini wewe wasema: ‘Hakuna tumaini lolote.Nimeipenda miungu ya kigeni,hiyo ndiyo nitakayoifuata.’

26. “Kama vile mwizi aonavyo aibu akishikwa,ndivyo Waisraeli watakavyoona aibu;wao wenyewe, wafalme wao, wakuu wao,makuhani wao na manabii wao.

27. Hao huuambia mti: ‘Wewe u baba yangu,’na jiwe: ‘Wewe ndiwe uliyenizaa;’kwa maana wamenipa kisogo,wala hawakunielekezea nyuso zao.Lakini wakati wa shida husema: ‘Inuka utuokoe!’

Yeremia 2