Yeremia 2:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu likanijia:

2. “Nenda ukawatangazie waziwazi wakazi wote wa Yerusalemu kuwa mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Naukumbuka uaminifu wako ulipokuwa kijana,jinsi ulivyonipenda kama mchumba wako,ulivyonifuata jangwanikwenye nchi ambayo haikupandwa kitu.

3. Israeli, wewe ulikuwa mtakatifu kwangu,ulikuwa matunda ya kwanza ya mavuno yangu.Wote waliokudhuru walikuwa na hatia,wakapatwa na maafa.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

4. Sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu, enyi wazawa wa Yakobo. Sikilizeni enyi jamaa zote za wazawa wa Israeli.

Yeremia 2