Yeremia 16:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia na kusema:

2. “Wewe hutaoa wala hutapata watoto mahali hapa.

3. Maana mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi juu ya watoto wa kiume na wa kike watakaozaliwa mahali hapa, na juu ya wazazi wao:

4. Hao watakufa kwa maradhi mabaya, na hakuna atakayewaombolezea wala kuwazika. Maiti zao zitazagaa kama mavi juu ya ardhi. Wataangamia kwa upanga na kwa njaa; na maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wakali wa nchi.

Yeremia 16