Yeremia 14:20-22 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Tunakiri uovu wetu, ee Mwenyezi-Mungu,tunakiri uovu wa wazee wetu,maana, tumekukosea wewe.

21. Usitutupe, kwa heshima ya jina lako;usikidharau kiti chako cha enzi kitukufu.Ukumbuke agano ulilofanya nasi, wala usilivunje.

22. Je miungu ya uongo ya mataifayaweza kuleta mvua?Au, je, mbingu zaweza kutoa manyunyu?Je, si wewe ee Mwenyezi-Mungu uliye Mungu wetu?Tunakuwekea wewe tumaini letu,maana wewe unayafanya haya yote.

Yeremia 14