20. Tunakiri uovu wetu, ee Mwenyezi-Mungu,tunakiri uovu wa wazee wetu,maana, tumekukosea wewe.
21. Usitutupe, kwa heshima ya jina lako;usikidharau kiti chako cha enzi kitukufu.Ukumbuke agano ulilofanya nasi, wala usilivunje.
22. Je miungu ya uongo ya mataifayaweza kuleta mvua?Au, je, mbingu zaweza kutoa manyunyu?Je, si wewe ee Mwenyezi-Mungu uliye Mungu wetu?Tunakuwekea wewe tumaini letu,maana wewe unayafanya haya yote.