Yeremia 13:23-27 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Je, Mwethiopia aweza kubadili rangi yake,au chui madoadoa yake?Ikiwezekana, nanyi pia mnaweza kutenda mema,nyinyi mliozoea kutenda maovu!

24. Mwenyezi-Mungu atawatawanya kama makapiyanayopeperushwa na upepo kutoka jangwani.

25. Mwenyezi-Mungu asema:“Hayo ndiyo yatakayokupata,ndivyo nilivyoamua kukutenda mimi Mwenyezi-Mungu,kwa sababu umenisahau mimi,ukaamini miungu ya uongo.

26. Nitalipandisha vazi lako hadi kichwanina aibu yako yote itaonekana wazi.

27. Nimeyaona machukizo yako:Naam, uzinifu wako na uzembe wako,na uasherati wako wa kupindukia,juu ya milima na mashambani.Ole wako ee Yerusalemu!Mpaka lini utakaa bila kutakaswa?”

Yeremia 13