8. Wote ni wajinga na wapumbavumafunzo ya vinyago ni upuuzi mtupu!
9. Vinyago hivyo hupambwa kwa fedha kutoka Tarshishi,na dhahabu kutoka Ofiri;kazi ya mafundi stadi na wafua dhahabu.Zimevishwa nguo za samawati na zambarau,zilizofumwa na wafumaji stadi.
10. Lakini Mwenyezi-Mungu ni Mungu wa kweli;Mungu aliye hai, mfalme wa milele.Akikasirika, dunia hutetemeka,mataifa hayawezi kustahimili hasira yake.
11. Basi, utawaambia hivi: “Miungu ambayo haikuumba mbingu na dunia, itaangamia. Itatoweka kabisa duniani na chini ya mbingu.”
12. Mwenyezi-Mungu aliiumba dunia kwa nguvu zake;kwa hekima yake aliuimarisha ulimwengu,kwa akili yake alizitandaza mbingu.