Yeremia 10:22-25 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Sikilizeni sauti! Habari zinatufikia.Kuna kishindo kutoka kaskazini.Taifa kutoka kaskazini linakuja,kuifanya miji ya Yuda kuwa jangwaambamo kutakuwa na mapango ya mbweha!

23. Najua, ee Mwenyezi-Mungu,binadamu hana uwezo na maisha yake;hakuna mtu awezaye kuyaongoza maisha yake.

24. Utukosoe, ee Mwenyezi-Mungu, lakini si kwa ghadhabu,wala kwa hasira yako, tusije tukaangamia.

25. Imwage hasira yako juu ya mataifa yasiyokuabudu,na juu ya watu ambao hawakutambui.Maana, wamewaua wazawa wa Yakobo;wamewaua na kuwaangamiza kabisa,na nchi yao wameiacha magofu.

Yeremia 10