Yakobo 4:14-17 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Nyinyi hamjui hata maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Nyinyi ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena.

15. Mngalipaswa kusema: “Bwana akitujalia tutaishi na tutafanya hiki au kile.”

16. Lakini sasa mwajivuna na kujigamba; majivuno ya namna hiyo ni mabaya.

17. Basi, mtu ambaye hafanyi lile jambo jema analojua kwamba anapaswa kulifanya, anatenda dhambi.

Yakobo 4