14. Nyinyi hamjui hata maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Nyinyi ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena.
15. Mngalipaswa kusema: “Bwana akitujalia tutaishi na tutafanya hiki au kile.”
16. Lakini sasa mwajivuna na kujigamba; majivuno ya namna hiyo ni mabaya.
17. Basi, mtu ambaye hafanyi lile jambo jema analojua kwamba anapaswa kulifanya, anatenda dhambi.