Waroma 2:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Na wewe, je? Wewe mwenyewe unajiita Myahudi; unaitumainia sheria na kujivunia kuwa wa Mungu;

18. kwa njia ya sheria unajua matakwa ya Mungu na unaweza kuchagua jambo jema;

19. wewe unajiona kuwa kiongozi wa vipofu na mwanga kwa wale walio gizani;

20. unajiona kuwa mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa wale wasiokomaa bado. Unayo katika sheria picha kamili ya elimu na ukweli.

Waroma 2