17. Na wewe, je? Wewe mwenyewe unajiita Myahudi; unaitumainia sheria na kujivunia kuwa wa Mungu;
18. kwa njia ya sheria unajua matakwa ya Mungu na unaweza kuchagua jambo jema;
19. wewe unajiona kuwa kiongozi wa vipofu na mwanga kwa wale walio gizani;
20. unajiona kuwa mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa wale wasiokomaa bado. Unayo katika sheria picha kamili ya elimu na ukweli.