Waroma 15:7-10 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Basi, karibishaneni kwa ajili ya utukufu wa Mungu kama naye Kristo alivyowakaribisheni.

8. Maana, nawaambieni Kristo aliwatumikia Wayahudi apate kuonesha uaminifu wa Mungu, na zile ahadi Mungu alizowapa babu zetu zipate kutimia;

9. ili nao watu wa mataifa mengine wapate kumtukuza Mungu kwa sababu ya huruma yake. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:“Kwa hiyo nitakusifu miongoni mwa watu wa mataifa.Nitaziimba sifa za jina lako.”

10. Tena Maandiko yasema:“Furahini, enyi watu wa mataifa;furahini pamoja na watu wake.”

Waroma 15