26. Tena, kamwe msile damu yoyote ile, iwe ya ndege au ya mnyama mahali popote mnapoishi.
27. Mtu yeyote akila damu yoyote, atatengwa na watu wake.”
28. Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose,
29. “Waambie watu wa Israeli hivi: Mtu yeyote akitoa sadaka ya amani, atampa Mwenyezi-Mungu sehemu ya sadaka hiyo.