Walawi 26:7-15 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Mtawafukuza adui zenu na kuwaua kwa upanga.

8. Watano wenu watawafukuza adui 100 na 100 wenu watawafukuza adui 10,000. Adui zenu wataangamia mbele yenu kwa upanga.

9. Nitawafadhili na kuwajalia mpate watoto wengi na kuongezeka; nami nitaliimarisha agano langu nanyi.

10. Wakati wa mavuno mtakuwa bado mnakula mazao ya zamani; tena itawalazimu kuondoa yaliyobaki kupata nafasi ya kuhifadhi mavuno mapya.

11. Nitaweka maskani yangu miongoni mwenu, wala sitawaacheni.

12. Nitatembea kati yenu na kuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu.

13. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, niliyewatoa nchini Misri ili msiwe watumwa wa Wamisri. Mimi nimevunja nira mliyofungiwa shingoni mwenu na kuwafanya mtembee wima.

14. “Lakini kama hamtanisikiliza wala kufuata amri zangu,

15. kama mkidharau masharti yangu na kuchukia kwa roho maagizo yangu mkaacha kuzitii amri zangu zote na kuvunja agano langu,

Walawi 26