Walawi 14:53-57 Biblia Habari Njema (BHN)

53. Yule ndege hai atamwacha aende zake mashambani nje ya mji. Hivyo ndivyo atakavyoitakasa nyumba hiyo, nayo itakuwa safi.”

54. Hii ndiyo sheria kuhusu aina yoyote ya namna ya upele wa ukoma;

55. upele katika nguo au nyumba,

56. uvimbe, jipu au kipaku,

57. ili kuonesha ni kitu gani kilicho najisi na kisicho najisi. Hiyo ndiyo sheria kuhusu namna ya upele wa ukoma.

Walawi 14