Walawi 11:11-18 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Viumbe hivyo vitakuwa daima najisi kwenu. Msile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao kwani ni najisi.

12. Chochote kinachoishi majini ambacho hakina mapezi na magamba ni najisi kwenu.

13. “Ndege wote wafuatao ni najisi kwenu; hivyo msile: Tai, furukombe, kipungu,

14. mwewe, aina zote za kozi,

15. aina zote za kunguru,

16. mbuni, kirukanjia, dudumizi, aina zote za kipanga,

17. bundi, mnandi, bundi kubwa,

18. mumbi, mwari, mderi,

Walawi 11