18. Ndiyo maana hata lile agano la kwanza halikuwekwa bila damu kumwagwa.
19. Kwanza Mose aliwatangazia watu wote amri zote kama ilivyokuwa katika sheria; kisha akachukua damu ya ndama pamoja na maji, na kwa majani ya mti wa husopo na pamba nyekundu, akakinyunyizia kile kitabu cha sheria na watu wote.
20. Mose alisema: “Hii ni damu inayothibitisha agano mliloamriwa na Mungu mlitii.”
21. Vilevile Mose aliinyunyizia damu ile hema na vyombo vya ibada.
22. Naam, kadiri ya sheria karibu kila kitu chaweza kutakaswa kwa damu, na dhambi nazo zaondolewa tu ikiwa damu imemwagwa.
23. Vitu hivi ambavyo ni mfano tu wa mambo halisi ya mbinguni, vililazimika kutakaswa kwa namna hiyo. Lakini vitu vya mbinguni huhitaji tambiko iliyo bora zaidi.