Waamuzi 9:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Kisha miti ikauambia mtini, ‘Njoo wewe utawale juu yetu.’

11. Lakini mtini ukajibu, ‘Je, mnadhani naweza kuacha shughuli yangu ya kuzalisha matunda mazuri na matamu, niende kujisumbua kuitawala miti?’

12. Halafu miti ikauambia mzabibu, ‘Njoo wewe uwe mtawala juu yetu.’

13. Lakini mzabibu ukajibu, ‘Mnadhani naweza kuacha shughuli yangu ya kuzalisha divai ambayo hufurahisha miungu na wanadamu, niende kujisumbua kuitawala miti?’

Waamuzi 9