Ufunuo 9:20-21 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Wanadamu wengine waliobaki ambao hawakuuawa na mabaa hayo, hawakutubu na kuviacha vitu walivyokuwa wametengeneza kwa mikono yao wenyewe; wala kuacha kuabudu pepo, sanamu za dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti, vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia wala kutembea.

21. Wala hawakutubu na kuacha kufanya mauaji, uchawi, uzinzi, na wizi.

Ufunuo 9