Nehemia 9:5-7 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Walawi, yaani: Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabuea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakawaambia watu;“Simameni na kumsifu Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.Msifuni milele na milele!Na watu walisifu jina lako tukufu,ambalo hutukuka kuliko baraka na sifa zote.”

6. Ezra akaomba kwa sala ifuatayo:“Wewe peke yako ndiwe Mwenyezi-Mungu;ndiwe uliyefanya mbingu na jeshi lake lote,dunia na vyote vilivyomo,bahari na vyote vilivyomo;nawe ndiwe unayevihifadhi hai,na jeshi lote la mbinguni lakuabudu wewe.

7. Wewe ndiwe Mwenyezi-Mungu,Mungu uliyemchagua Abramu,ukamtoa toka Uri ya Wakaldayona kumpa jina Abrahamu.

Nehemia 9