Mwanzo 49:14-19 Biblia Habari Njema (BHN)

14. “Isakari ni kama punda mwenye nguvu,ajilazaye kati ya mizigo yake.

15. “Aliona kuwa mahali pa kupumzikia ni pema,na kwamba nchi ni ya kupendeza,akauinamisha mgongo wake kubeba mzigo,akawa mtumwa kufanya kazi za shuruti.

16. “Dani atakuwa mwamuzi wa watu wake,kama mojawapo ya makabila ya Israeli.

17. “Atakuwa kama nyoka njiani,nyoka mwenye sumu kando ya njia,aumaye visigino vya farasi,naye mpandafarasi huanguka chali.

18. “Ee Mwenyezi-Mungu, nangojea uniokoe!

19. “Gadi atashambuliwa na wanyanganyi,lakini yeye atawafuata nyuma na kuwashambulia.

Mwanzo 49