Mwanzo 44:3-6 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Kulipopambazuka wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda wao.

4. Walipokuwa wamesafiri mwendo mfupi tu kutoka mjini, Yosefu alimwambia msimamizi wa nyumba yake, “Haraka! Wafuate wale watu, na utakapowakuta, uwaulize, ‘Kwa nini mmelipa mema mliyotendewa kwa maovu? Kwa nini mmeiba kikombe cha bwana wangu ambacho

5. yeye hunywa nacho na kukitumia kupiga ramli? Mmekosa sana kwa kufanya hivyo!’”

6. Yule msimamizi alipowakuta akawaambia maneno haya.

Mwanzo 44