Mwanzo 41:28-30 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Kama nilivyokueleza, ee Farao, Mungu amekufunulia mambo atakayofanya hivi karibuni.

29. Kutakuwa na miaka saba ya shibe katika nchi nzima ya Misri.

30. Lakini baadaye itafuata miaka saba ya njaa, hata hiyo shibe isahaulike kabisa. Njaa hiyo itaiangamiza nchi hii.

Mwanzo 41