Mwanzo 32:24-27 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Yakobo alibaki peke yake. Mtu mmoja akaja, akapigana naye mwereka mpaka alfajiri.

25. Mtu huyo alipoona kwamba hawezi kumshinda Yakobo, alimgusa Yakobo nyonga ya kiuno, naye akateguka alipokuwa anapigana naye mwereka.

26. Kisha yule mtu akamwambia Yakobo, “Niache niende zangu, kwani kunapambazuka.” Lakini Yakobo akamwambia, “Sikuachi kamwe, mpaka umenibariki!”

27. Naye akamwuliza, “Jina lako nani?” Yeye akamjibu, “Yakobo.”

Mwanzo 32