Mwanzo 32:20-27 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Zaidi ya yote, mtamwambia, ‘Mtumishi wako Yakobo yuko nyuma, anafuata.’” Yakobo alifanya hivyo akifikiri, “Pengine nitamtuliza kwa zawadi hizi ninazomtangulizia, na baadaye naweza kuonana naye ana kwa ana; huenda atanipokea.”

21. Basi, akatanguliza zawadi zake, lakini yeye mwenyewe akalala kambini usiku huo.

22. Usiku huohuo Yakobo akaamka, akawachukua wake zake wawili, wajakazi wake wawili na watoto wake kumi na mmoja, akapita kivuko cha Yaboki.

23. Baada ya kuwavusha ngambo ya kijito wale waliokuwa nao na mali yake yote,

24. Yakobo alibaki peke yake. Mtu mmoja akaja, akapigana naye mwereka mpaka alfajiri.

25. Mtu huyo alipoona kwamba hawezi kumshinda Yakobo, alimgusa Yakobo nyonga ya kiuno, naye akateguka alipokuwa anapigana naye mwereka.

26. Kisha yule mtu akamwambia Yakobo, “Niache niende zangu, kwani kunapambazuka.” Lakini Yakobo akamwambia, “Sikuachi kamwe, mpaka umenibariki!”

27. Naye akamwuliza, “Jina lako nani?” Yeye akamjibu, “Yakobo.”

Mwanzo 32