Mwanzo 31:4-6 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Basi Yakobo akataka Raheli na Lea waitwe; nao wakamwendea mbugani alikokuwa anachunga wanyama.

5. Yakobo akawaambia, “Naona kuwa baba yenu hanijali tena kama hapo awali. Lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami.

6. Mnajua kwamba nimemtumikia baba yenu kwa nguvu zangu zote.

Mwanzo 31