Mwanzo 27:37-40 Biblia Habari Njema (BHN)

37. Isaka akamjibu, “Nimekwisha mfanya Yakobo kuwa mtawala wako, na kumpa ndugu zake wote kuwa watumishi wake. Nimempatia nafaka na divai. Nikufanyie nini sasa, wewe mwanangu?”

38. Esau akamwambia baba yake, “Baba, kwani una baraka moja tu? Nibariki hata mimi, ee baba!” Hapo Esau akalia kwa sauti kubwa.

39. Ndipo Isaka, baba yake, akamwambia,“Makao yako yatakuwa mbali na ardhi yenye rutuba,na mbali na umande wa mbinguni.

40. Utaishi kwa upanga wako,na utamtumikia ndugu yako;lakini utakapoasiutaivunja kongwa yake shingoni mwako.”

Mwanzo 27