Mwanzo 27:24-27 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Akamwuliza tena, “Kweli wewe ndiwe mwanangu Esau?” Naye akamjibu, “Ndiyo.”

25. Basi, baba yake akasema, “Niletee hiyo nyama nile mawindo yako mwanangu, nikubariki.” Hapo Yakobo akampelekea chakula, naye akala; akampelekea divai pia, akanywa.

26. Ndipo baba yake Isaka, akamwambia, “Sogea karibu, mwanangu, unibusu.”

27. Basi, Yakobo akamkaribia baba yake na kumbusu, na baba yake aliposikia harufu ya mavazi yake, akambariki akisema,“Tazama, harufu nzuri ya mwananguni kama harufu ya shamba alilobariki Mwenyezi-Mungu!

Mwanzo 27