14. Basi, Yakobo akaenda, akachukua wanambuzi wawili, akamletea mama yake; naye akatayarisha chakula kitamu, kile apendacho Isaka baba yake.
15. Kisha Rebeka akatwaa mavazi bora ya Esau, mwanawe mkubwa, aliyokuwa nayo nyumbani, akamvika Yakobo, mwanawe mdogo.
16. Akamvika pia ngozi za wale wanambuzi mikononi na kwenye sehemu laini shingoni mwake.
17. Kisha akampa kile chakula kitamu na mkate aliokuwa ametayarisha.
18. Basi, Yakobo akaingia ndani kwa baba yake, akamwita, “Baba!” Naye akaitika, “Naam! Ni nani wewe mwanangu?”