Mwanzo 25:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Abrahamu alioa mke mwingine, jina lake Ketura.

2. Ketura alimzalia Abrahamu: Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua.

3. Yokshani alimzaa Sheba na Dedani; wazawa wa Dedani walikuwa Waashuru, Waletushi na Waleumi.

4. Watoto wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Henoki, Abida na Eldaa. Wote hao walikuwa wazawa wa Ketura.

Mwanzo 25