Mwanzo 24:28-30 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Kisha yule msichana akakimbia kwenda kuwapa habari jamaa za mama yake.

29. Rebeka alikuwa na kaka yake aitwaye Labani. Labani akatoka mbio kukutana na yule mtu kisimani.

30. Labani alikuwa ameiona ile pete na bangili mikononi mwa dada yake, na kusikia mambo Rebeka aliyoambiwa na huyo mtu. Labani alimkuta yule mtu amesimama karibu na ngamia wake kando ya kisima.

Mwanzo 24