Mwanzo 21:2-5 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Basi, Abrahamu akiwa mzee, Sara akapata mimba, akamzalia mtoto wa kiume, wakati uleule Mungu alioutaja.

3. Abrahamu akampa huyo mwanawe ambaye Sara alimzalia jina Isaka.

4. Isaka alipotimiza umri wa siku nane, Abrahamu akamtahiri kama alivyoamriwa na Mungu.

5. Abrahamu alikuwa na umri wa miaka 100 wakati mwanawe Isaka alipozaliwa.

Mwanzo 21