1. Mwenyezi-Mungu alimkumbuka Sara, akamtendea kama alivyoahidi.
2. Basi, Abrahamu akiwa mzee, Sara akapata mimba, akamzalia mtoto wa kiume, wakati uleule Mungu alioutaja.
3. Abrahamu akampa huyo mwanawe ambaye Sara alimzalia jina Isaka.
4. Isaka alipotimiza umri wa siku nane, Abrahamu akamtahiri kama alivyoamriwa na Mungu.