22. Harakisha! Kimbilia huko, nami sitafanya lolote mpaka utakapowasili huko.” Hivyo mji huo ukaitwa Soari.
23. Jua lilikuwa limekwisha chomoza wakati Loti alipowasili mjini Soari.
24. Ndipo Mwenyezi-Mungu akateremsha moto mkali wa kiberiti kutoka mbinguni juu ya Sodoma na Gomora,
25. akaiangamiza miji hiyo, bonde lote, wakazi wake wote na mimea yote katika nchi hiyo.